SEMINA YA VIONGOZI DINI, VYAMA VYA
SIASA, VYOMBO VYA DOLA NA VYOMBO VYA SHERIA.
MADA
UMUHIMU WA AMANI NA UTULIVU KATIKA JAMII
Imeandaliwa na:
Sheikh Abdulla Talib Abdulla Kamisheni ya Wakf na
UTANGULIZI:
Sifa njema zote anastahiki Mwenyezi Mungu
amabe kwa uwezo wake na nguvu zake tuweweza kukusanyika hapa ili kujadili swala
muhimu linaloihusu jamii yetu nalo ni kudumisha amani na utulivu. Sala na salam
zimshukie Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na wafuasi wake wote hadi siku ya kiama.
Aidha natowa shukrani zangu za dhati kabisa kwa wale wote waliochangia kwa
namna moja au nyengine katika kufanikisha mkusanyiko huu. Ninamuomba Mwenyezi
Mungu aziweke juhudi zao hizo katika mizani ya mema
Amesema mwanachuoni Ibnu Khaldoun: “Kwa hakika kuwepo jamii ya mwanadamu
ni jambo la msingi na la umuhimu mno, kwani binadamu ni mwanajamii katika
maumbile yake, anazaliwa katika jamii, anaishi na kufia humo”.
Kwa msingi huo, ikiwa jamii ni jambo la
lazima kwa mwanadamu ambalo haepukani nalo, nayo ndio inayojenga mustakabali na
hadhi ya mwanadamu kuanzia kwake binafsi na mbele ya jamii nyengine basi ni
lazima jamii hiyo itunzwe na ienziwe ili idumu katika uasili wake ambao ni
mapenzi, amani, utulivu na umoja. Amesema Mwenyezi Mungu: ((Enyi watu mcheni Mola wenu ambae
amekuumbeni kutokana na nafsi moja, na akaumba katika nafsi hiyo mkewe, na
akaeneza kwa wawili hao wanaume wengi na wanawake wengi)) {Suratul Nisai aya ya 1} Na akasema tena ((Kwa
hakika sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamme mmoja na mwanamke mmoja na
tukakujaalieni mataifa na makabila mbali mbali ili mjuane, hakika mbora wenu
mbele ya Allah ni yule mchaji zaidi)) {Suratul Alhujurati aya ya
13}.
Jamii yetu imejengwa na wafuasi wa
itikadi, imani na mitizamo tofauti katika nyanja za dini, siasa, fikra n.k.
mambo haya yamo ndani ya nyoyo zetu na ni katika uhuru aliotupa Muumba wa
kujichagulia njia tunayopenda
Dini ni mfumo na utaratibu wa maisha
uliowekwa na Muumba ili kutawala maisha ya mwanadamu. Kwa vile mwanadamu ni
mwanajamii kwa maumbile yake ni lazima awekewe mfumo na utaratibu unaoeleweka
unaoongoza mwenendo wa jamii hiyo na kulinda maslahi ya wanajamii wote.
Kutokuwepo kutokufuatwa au kutokusimamiwa vyema mfumo huu na wanajamii hasa
wenye mamlaka ya uongozi kutapelekea kutoweka kwa amani na utulivu katika jamii
na badala yake jamii itaishi
Uislamu ukiwa ni katika mifumo ya maisha
umeweka utaratibu ambao unachunga maisha ya wanajamii na ulimwengu mzima waishi
kwa amani na utulivu ambao umejengwa juu ya msingi wa itikadi ya kumpwekesha
Mwenyezi Mungu yaani tawhidi. Msingi unamuainisha kila mwanadamu katika jamii,
cheo chake (utukufu wake), lengo la kuumbwa kwake, na mahusiano yake na Muumba
na vyote vilivyomo duniani. Itikadi ndio ilani na dira ambayo inatakiwa iongoze
fikra na matendo ya mtu aliyejikubalisha kuwa muislamu na kuongoza kila jambo
lake la siri na dhahiri.
Itikadi ya kiislamu imeweka mambo matano
ambayo yanatakiwa kuchugwa
· Kuhifadhi dini
· Kuhifadhi nafsi (maisha ya mwanadamu)
· Kuhifadhi
· Kuhifadhi heshima za watu
· Kuhifadhi akili
KUHIFADHI DINI:
Dini kama tulivyotangulia kuieleza ni
mfumo wa maisha. Mfumo huu unakusanya itikadi sheria na tabia. Uislamu
umesisitiza itikadi ipandikizwe, sheria zisimamiwe na tabia ziendelezwe ili
dini ipate kudumu, kuhifadhika na kuleta maslahi kwa wanajamii.
Kwa mnasaba wa mkusanyiko wetu huu, jamii
yetu imejiwekea mfumo uliowazi na unaoeleweka ambao unatoa haki, majukumu, na
kupanga mahusiano na maingiliano ya wanajamii, mipaka hii ndio inayotakiwa
ielekeze tabia na mienendo ya wanajamii wote.
Kila mmoja kati yetu anahusika kwa namna
fulani katika uanzishwaji, usimamizi na utekelezaji wa mfumo huu. Na mafunzo ya
dini yanatufunza kuwa ataulizwa na Mwenyezi Mungu ni kwa namna gani ameisimamia
dhamana yake
Tukiwa ni viongozi tuliopewa hatamu na
tuangalie vyema wapi tunaipeleka jamii yetu na kwa faida ya nani? Tujiepushe na
kufuata matamanio ya nafsi zetu ili tufuate sheria na taratibu zilizopo huku
tukizingatia kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema: ((Na lau
KUHIFADHI NAFSI:
Nafsi ya mwanadamu imetukuzwa
Ikiwa hali ndio
Tutambue kuwa sote ni watu wa jamii moja
na asili ya wanaadamu wote ni moja
Mwenyezi Mungu kwa kumtukuza mwanadamu
amempa akili na kipaji ili aweze kujiletea maslahi katika dunia yake na akhera
yake. Hivyo akili yake inapomuongoza katika itikadi, fikra, mtizamo tofauti na
ulizonazo wewe tunatakiwa kuvumiliana au kushindana kihoja na kujiepusha na
kila litakaloleta madhara
Mwenyezi Mungu amrehemu Sayyidna Omar
aliposema “lau
KUHIFADHI
Ikiwa kuhifadhi amani na utulivu katika
jamii yetu suala la mgawanyo wa rasilimali za taifa ni lazima lizingatiwe
Mali ikiwa ni kidogo au nyingi ina
thamani kubwa kwa mwenyewe na kuharibiwa kwake kuna athari mbaya sana, motokeo
ya kuchomwa moto nyumba, kuharibiwa mazao au mali za watu binafsi na serikali
limekuwa ni jambo la kawaida katika kipindi kama hiki, lakini ukitafakari ni
kwa faida ya nani? Jamii inapokuwa na watu wenye nguvu kiuchumi n.k. ndiyo nayo
inavyokuwa na nguvu kiuchumi, kijamii na kuweza kuziathiri jamii nyengine.
Vinginevyo itazidi kuwa dhaifu na kuathiriwa na jamii nyenginezo zenye nguvu
katika kila nyanja.
Tukiwa ni viongozi na wenye dhamana
muhimu katika taasisi zetu tujitahidi kulinda
Hivyo katika kuhifadhi
KUHIFADHI HESHIMA ZA WATU:
Dini inatutaka kuheshimiana na
kutodharauliana kwa itikadi, uwezo fikra, mitizamo n.k. Tunatakiwa tuwaheshimu
watu kwa vile ni binadamu alietukuzwa mbele ya Mwenyezi Mungu, na ana haki na
uhuru wa kufuata mtizamo mwengine au kufanya tendo lolote madhali hatokiuka
sheria na taratibu zilizopo.
Kwa msingi huu dini imeweka kipimo cha
uadilifu kuwa ndio kinachonyanyua shakhsia ya mtu au kikundi na sio ukoo,
kabila, jimbo, jinsi, chama au itikadi. Aidha dini imesisitiza tabia njema na
kukataza yote yanayovunja heshima za watu, ikiwemo kudhalilishwa, kusingiziwa
uongo, kusengenywa, kutukanwa n.k. Amesema Mtume S. A. W: ((Kumtukana muumini ni ufasiki na
kumpiga ni ukafiri)).
Katiba za nchi yetu na miongozo ya vyama
na taasisi zetu zinaamini na kuahidi kutetea haki za binaadamu hivyo kila mmoja
wetu na atekeleze wajibu wake ili kuhakikisha kuwa amani na utulivu unadumishwa
kwa maslahi ya jamii nzima. Tulinganie sera zetu kwa kadiri ya uwezo wetu na
tuwe tayari kusahihishana na kurekebishana kwani hakuna mkamilifu isipokuwa
Mwenyezi Mungu. Hata hivyo kusahihishana, kukosoana na kuelekezana ni lazima
kuwe kwa heshima na meneno mazuri na sio vyenginevyo kwani sote tuko kwenye
jahazi moja na likitoboka tutaghariki sote.
KUHIFADHI AKILI:
Akili ni nyenzo ambayo inamtofautisha
mwanadamu na mnyama kwa vile ndio inayomuwezesha kufikiri. Akili inatakiwa
kuhifadhiwa kwa kukuzwa kielimu na kimaarifa. Vile vile kukingwa na yote
yatakayoweza kuifisidi na ndio maana ukaharamishwa ulevi wa namna zote na
mafunzo yote mabaya.
Mwenyezi Mungu ametupa dhamana katika
jamii yetu, wanajamii wanatufuata na kutusikiliza hivyo ni lazima tuwe makini
katika yale tunayoyapandikiza kwa wafuasi tusije tukapotea au kupoteza. Amesema
Mtukufu ((Jee ndio
yanayotarajiwa kwenu wakati mkipata ukubwa kufisidi katika ardhi na kuwakata
jamaa)) Muhammad aya ya 22.
Tutambue kuwa sera na matendo yetu yatakapokwenda kinyume na maamrisho ya dini Mwenyezi Mungu hatotuacha
Migogoro ni sababu kubwa ya kudumaa na
kuvia maendeleo ya jamii yoyote. Jamii inapokosa amani na utulivu migogoro na
fujo ndio hushika hatamu na jamii huporomoka katika kila nyanja na kudharaulika
mbele ya jamii nyengine. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu ((Wala msizozane (msigombane) msije
mkaharibikiwa na kupotea nguvu zenu, na vumilieni (mstahamiliane) bila shaka
Mwenyezi Mungu yu pamoja na wanaovumilia))
{Al-Anfal aya ya 46).
Katika karne tuliyonayo ya sayansi na
teknolojia ulimwengu umekuwa
Dunia imeshuhudia walimwengu wakikimbiana
katika nguvu za kielimu, kisiasa, kiuchumi na kuitamaduni. Wazanzibari na
Watanzania hatukusalimika katika kinyang’angiro hicho nasi tuna nafasi kubwa ya
kuipeleka mbele jamii yetu au huisababisha kubanwa kipembeni na kutoweza
kupumua vyema.
Ni lazima tufikiri mara nyingi kabla ya
kusema au kutenda tuweke mbele maslahi ya nchi na watu wetu, tujuwe kuwa
matendo yetu yatasajiliwa na historia na kizazi kijacho kitatuhukumu kwayo ima
vyema au vibaya. Na mwisho wa maisha yetu mafupi ni kuingia kaburini kuanza
maisha ya milele. Mauti yatatuenea sote, kaburi litatubana sote na kwa Mwenyezi
Mungu tutarejeshwa sote akatuhukumu kwa haki nae ni mbora wa mahakimu.
Tunamuomba Allah atupe amani na utulivu
katika nchi yetu.